BUKOBA SPORTS

Monday, February 2, 2015

AFCON: CÔTE D'IVOIRE 3 vs 1 ALGERIA, WILFRIED BONNY ATUPIA MARA MBILI WAKISONGA NUSU FAINALI!

CÔTE D'IVOIRE
W. Bony 26 na dakika ya 68
Y. Gervinho alimalizia dakika ya 90 na Mtanange kumalizika 3-1

Ivory Coast players celebrate
ALGERIA
E. Soudani aliifungia bao pekee dakika ya 51 kipindi cha pili.

Huko Nuevo Estadio de Malabo, Mjini Malabo Nchini Equatorial, Mchezaji mpya wa Manchester City, Wilfried Bony, na yule wa zamani wa Arsenal, Gervinho, ambae sasa yupo AS Roma walipachika Mabao yaliyoipeleka Nchi yao Ivory Coast Nusu Fainali ya AFCON 2015, Kombe la Mataifa ya Afrika, walipoitwanga Algeria Bao 3-1.
Bony alifunga Bao la kwanza Dakika ya 26 kwa Kichwa alipounganisha Krosi ya Max Gradel lakini Hilal Soudani akaisawazishia Algeria Dakika ya 51 na ndipo Bony akafunga tena kwa Kichwa Bao la Pili alipounganisha Frikiki ya Yaya Toure katika Dakika ya 69.
Bao la 3 lilifungwa na Gervinho katika Dakika ya 90.
Kwenye Nusu Fainali, Jumatano ni Congo DR v Ivory Coast na Alhamisi ni Equatorial Guinea v Ghana.

No comments:

Post a Comment