BUKOBA SPORTS

Thursday, February 5, 2015

FA CUP: LIVERPOOL YATINGA RAUNDI YA 5, YAIFUNGA BOLTON WAKIWA 10 KWA MBINDE DAKIKA ZA MAJERUHI!

BAO la Dakika ya 90 la Philippe Coutinho limeipeleka Liverpool Raundi ya 5 ya FA CUP walipotoka nyuma na kuifunga Bolton Wanderers Bao 2-1 Jana Usiku katika Mechi ya marudiano baada ya kutoka Sare huko Anfield katika Mechi ya kwanza.
Wakicheza kwao, Bolton walitangulia kufunga kwa Bao la Penati ya Dakika ya 59 la Gudjohnsen na Liverpool kusawazisha Mfungaji akiwa Raheem Sterling katika Dakika ya 86.
Bolton walicheza Mtu 10 kuanzia Dakika ya 66 baada ya Neill Danns kupewa Kadi Nyekundu.
Kwenye Raundi ya 5 Liverpool watacheza Ugenini na Crstal Palace.
Raheem Sterling akishangilia bao lake la kusawazisha kwa Liverpool.

No comments:

Post a Comment