BUKOBA SPORTS

Thursday, February 5, 2015

LA LIGA: REAL MADRID 2 - 1 SEVILLA, JAMES RDRIGUEZ AUMIA!! REAL IKIPAA KILELENI TENA!!

James Rodriguez Akifunga bao kwa kichwaBAO 2 za James Rodriguez na Jese Rodriguez zimewapa Real Madrid ushindi wa Bao 2-1 walipocheza kwao Santiago Bernabeu na Sevilla kwenye Mechi ya kiporo ya La Liga na kuwafanya waongoze kwa Pointi 4 mbele ya Barcelona.
Dakika ya 12 James Rodriguez aliwapa Bao Real Madrid na kisha Jese Ròdriguez, alieingia kuchukua nafasi ya James Rodriguez alievunjika kidolè cha mguu, kufunga Bao la Pili Dakika ya 36 huku Sevilla wakipata Bao lao Dakika ya 90 kupitia Iago Aspas.

Kwenye Mechi hiyo, Real walimkosa Supastaa wao Cristiano Ronaldo ambae alikuwa akimalizia Kifungo cha Mechi mbili baada ya kupewa Kadi Nyekundu.
Lakini Jumamosi Ronaldo atarejea kilingeni kwenye Dabi ya Jiji la Madrid huko Vicente Calderon wakati Real watakuwa Wageni wa Mahasimu zao Atletico Madrid kwenye Mechi ya La Liga.

No comments:

Post a Comment