Baada ya Mechi hiyo, Van Gaal aliongea: “Najua kwenye Mechi kama hizi kila kitu kinakupinga. Washabiki, Kiwanja na Difensi yao. Hata Refa, mlimwona. Kila kitu unachoweza kufikiria kinakupinga. Cambridge ni Timu dhaifu, kila Mtu anajua hilo, na lazima ujue namna ya kuwafunga. Lakini mara nyingi unashindwa. Kwa bahati bado tupo FA CUP. Tunacheza Nyumbani na lazima tuwafunge!”
Van Gaal amepewa hadi Saa 3 Usiku Jumatatu Februari 9 kujibu Mashitaka yake.
kwenye Marudiano, Man United iliitandika Cambridge United Bao 3-0 na kutinga Raundi ya 5 ya FA CUP na itacheza Ugenini na Preston North End hapo Februari 16.
No comments:
Post a Comment