
Safari hii, wakiwa kwao Nou Camp Jumanne Usiku, Barcelona kidogo watapata kashkash kwani PSG itaimarika kwa kuwemo baadhi ya Mastaa hao pamoja na Supastaa Zlatan Ibrahimovic aliekosa Mechi ya kwanza kwa kuwa Kifungoni.
Lakini, ili kufuzu, PSG wana kibarua kigumu cha kupata ushindi mnono ili kupiku Bao za Ugenini za Barcelona.
Jumatano Usiku, Juventus, walioshinda kwao Turin, Italy Bao 1-0, wako Ugenini kurudiana na AS Monaco.
Siku hiyo hiyo Jumatano, ipo El Derbi Madrileno, Dabi ya Jiji la Madrid, wakati Mahasimu Real Madrid na Atletico Madrid watakaporudiana huko Santiago Bernabeu huku matokeo ya Mechi ya kwanza yakiwa ni 0-0.
UEFA CHAMPIONS LEAGUE
Robo Fainali-Mechi za Marudiano
Mechi zote kuanza Saa 3 Dakika 45 Usiku
Jumanne Aprili 21
Bayern Munich vs FC Porto [Allianz Arena, Munich, Germany] (1-3)
Barcelona vs Paris Saint-Germain [Nou Camp, Barcelona, Spain] (3-1)
Jumatano Aprili 22
Real Madrid vs Atletico Madrid [Santiago Bernabeu, Madrid, Spain] (0-0)
AS Monaco vs Juventus [Stade Louis II, Monaco, France] (0-1)
No comments:
Post a Comment