BUKOBA SPORTS

Monday, April 20, 2015

UEFA CHAMPIONS LEAGUE: KUPIGWA JUMANNE NA JUMATANO WASHINDI KWENDA NUSU FAINALI!

Klabu 4 ambazo zitatinga Nusu Fainali ya UEFA CHAMPIONS zitapatikana Jumanne na Jumatano baada ya kukamilika kwa Mechi za Marudiano za Robo Fainali.
Baada ya Mechi za Kwanza za Robo Fainali, ni Barcelona pekee ipo hali njema baada ya kupata ushindi mnono wa Bao 3-1 Ugenini huko Paris, France walipoinyuka Paris Saint-Germain dhaifu iliyokosa Mastaa wake kadhaa.
Safari hii, wakiwa kwao Nou Camp Jumanne Usiku, Barcelona kidogo watapata kashkash kwani PSG itaimarika kwa kuwemo baadhi ya Mastaa hao pamoja na Supastaa Zlatan Ibrahimovic aliekosa Mechi ya kwanza kwa kuwa Kifungoni.
Lakini, ili kufuzu, PSG wana kibarua kigumu cha kupata ushindi mnono ili kupiku Bao za Ugenini za Barcelona.

Timu nyingine ambayo iliambua ushindi mnono ni FC Porto ya Ureno walipoichapa Bayern Munich 3-1 huko Mjini Porto lakini sasa Jumanne wako Ugenini Allianz Arena Jijini Munich ambako Bayern watasaka ushindi wa 2-0 ili wafuzu.
Jumatano Usiku, Juventus, walioshinda kwao Turin, Italy Bao 1-0, wako Ugenini kurudiana na AS Monaco.
Siku hiyo hiyo Jumatano, ipo El Derbi Madrileno, Dabi ya Jiji la Madrid, wakati Mahasimu Real Madrid na Atletico Madrid watakaporudiana huko Santiago Bernabeu huku matokeo ya Mechi ya kwanza yakiwa ni 0-0.

UEFA CHAMPIONS LEAGUE

Robo Fainali-Mechi za Marudiano
Mechi zote kuanza Saa 3 Dakika 45 Usiku
 
Jumanne Aprili 21
Bayern Munich vs FC Porto [Allianz Arena, Munich, Germany] (1-3)
Barcelona vs Paris Saint-Germain [Nou Camp, Barcelona, Spain] (3-1)
Jumatano Aprili 22
Real Madrid vs Atletico Madrid [Santiago Bernabeu, Madrid, Spain] (0-0)
AS Monaco vs Juventus [Stade Louis II, Monaco, France] (0-1)

No comments:

Post a Comment