David Beckhama, ambae pia alikuwa Kepteni wa Timu ya Taifa ya England, hayumo kwenye Listi hiyo ya Wachezaji hao Wanne ambao ni Cristiano Ronaldo, Ryan Giggs, Paul Scholes na Eric Cantona.
Akihojiwa na BBC, Shirika la Habari la Uingereza, kama kutokuwepo kwenye Listi hiyo ni ‘tusi’ kwake, Beckham alijibu: “Hapana kabisa.”
Alieleza: “Nimecheza chini ya Meneja Bora katika Historia yote kwa muda niliocheza, nilibahatika kucheza na Wachezaji niliocheza nao na kupata mafanikio makubwa kwa Klabu niliyoipenda na bado naipenda.”
Aliongeza: “Nakubaliana na Meneja. Wapo kwa hakika Wachezaji unaoweza kuwaita wa kiwango cha Dunia na nashukuru nilicheza na wengi wao.”

No comments:
Post a Comment