BUKOBA SPORTS

Saturday, October 24, 2015

LA LIGA: CELTA VIGO 1 v 3 REAL MADRID, RONALDO AIWEZESHA REAL KUKWEA KILELENI LEO!

Ronaldo akishangiliaCristiano Ronaldo mapema dakika ya 8' aliwapa Real bao na dakika ya 23 Danilo aliwaongezea bao na kufanya Real kuongoza bao kuwa 2-0 dhidi ya Celta Vigo.
Cristiano Ronaldo leo hii aliifungia Real Madrid Bao la kwanza wakati iliposhinda Ugenini Bao 3-1 walipocheza na Timu ya Pili kwenye La Liga Celta Vigo. 

Bao nyingine za Real zilifungwa na Danilo na Marcelo huku Bao la Celta Vigo likifungwa na Nolito.
Hadi Mapumziko Real walikuwa mbele 2-0 na kilipoanza tu Kipindi cha Pili Gustavo Cabral wa Celta Vigo alitolewa nje kwa Kadi Nyekundu baada ya kulambwa Kadi za Njano 2.


Ushindi huu wa Real, ambao bado inawakosa majeruhi Gareth Bale, Karim Benzema na James Rodriguez, umewapaisha na kuwa kileleni Pointi 3 mbele ya Timu ya Pili Celta Vigo na Barcelona.
Pongezi kutoka kwa MarceloRonaldo akichuana viikali na GonezNolito na da SilvaLuca Modric akimpongeza Danilo kwa kufunga baoDanilo akiomba kwa baoAugusto na Carlos Casemiro

No comments:

Post a Comment