Wadau wa Arsenal wamekuwa wakimpinga Wenger na kumtaka ang’oke kama Meneja baada ya kuona kwa mara nyingine tena wakianza vyema Msimu lakini baadae Timu ikisambaratika kwenye mbio za Ubingwa.
Wenger, ambae alitwaa Ubingwa wa England akiwa na Arsenal mara 3 na ya mwisho ikiwa 2004, amekiri kuelewa huzuni ya Mashabiki.
Lakini amesisitiza kuwa wapo Wachambuzi ambao hurubuni Mashabiki ili kusapoti upinzani ndani ya Klabu kwa maslahi na chuki zao binafsi.
Jumamosi, Arsenal wako kwao Emirates kucheza na Norwich City Mechi ambayo ni muhimu kwao kujihakikishia kuwemo 4 Bora za Ligi Kuu England ili kucheza UCL, UEFA CHAMPIONS LIGI Msimu ujao.
Kwenye Mechi hiyo, lipo kundi la Mashabiki wa Arsenal ambao wamepanga ‘kuandamana’ ili kuonyesha kupinga kwao uendeshwaji wa Klabu.
Aliongeza: “Ikiwa Klabu haiwezi kufurahia kitu chochote, basi ni mashaka. Kwenye Soka, unaporomoka haraka na unapanda polepole! Lazima tuwe kitu kimoja!”
No comments:
Post a Comment