
Leicester, chini ya Kocha kutoka Italy Claudio Ranieri, wanahitaji Pointi 3 tu kutwaa Ubingwa wao wa kwanza wa England katika Historia ya Miaka 132.
Lakini Man United, wakiwa wamebakiza Mechi 4 za BPL, bado wamo kwenye vita ya kuwania kutinga 4 Bora ili wacheze UEFA CHAMPIONZ LIGI Msimu ujao.

Man United v Leicester City KUKUTANA:
-Man United wamefungwa Mechi 1 tu kati ya 13 za mwisho dhidi ya Leicester na hiyo ilikuwa 5-3 Msimu uliopita huko King Power Stadium.
-Mechi ya mwisho kati ya Leicester na Man United ilichezwa Novemba 28 huko King Power Stadium na kuisha 1-1.
-Leicester, ambao wako kileleni mwa BPL kwa Siku zaidi ya 100, wamefungwa Mechi 1 tu kati ya 13 zilizopita.
Mbali ya kusema Ranieri na Leicester wanastahili Ubingwa, pia Van Gaal alieleza kuwa hilo ni jambo jema kwa England na Soka kwamba si Timu ile ile tu inatwaa Ubingwa.
Van Gaal ametamka: “Walipata nafasi ya kuchezesha Kikosi kilekile kwa vile hawakuwa na Mechi nyingi ukilinganisha na Timu nyingine. Ni jambo jema kwa Ligi Kuu na Soka kwamba si Timu ile ile tu inatwaa Ubingwa siku zote!”
No comments:
Post a Comment