Mfaransa huyo amesema hajali kuhusu kundi kubwa la Washabiki wa Klabu hiyo wenye Tiketi za Msimu mzima kuhudhuria Mechi za Nyumbani za Uwanjani Emirates kuzimwaga Tiketi zao na kuruhusu nafasi zao ziuzwe upya.
Kitendo hicho ni wazi Mashabiki wamechukizwa na mwendo wa Arsenal.
Katika Miezi ya hivi karibuni, Bango kubwa linalomtaka Wenger ang’oke Arsenal limekuwa litundikwa juu kwenye Mechi za Arsenal.
Wenger ameeleza: “Tizama, kila mtu yuko huru kuamua nini anafanya kwa Tiketi yake ya Msimu. Ni Mechi ya Alhamisi Usiku na hii si kawaida. Pia hatukupata matokeo mazuri Mechi iliyopita Nyumbani na pengine hiyo ni sababu! Lazima tuishi na hayo!”
No comments:
Post a Comment