Hili ni Taji la Pili Msimu huu kwa Bayern ambao pia wamebeba Ubingwa wa Bundesliga kwenye Msimu huu wa mwisho wa Guardiola anaehamia Manchester City na Bayern kutwaliwa na Meneja mpya Carlo Ancelotti.
Kwenye Fainali hii Gemu ilikuwa 0-0 hadi mwisho wa Dakika 90 na Nyongeza ya Dakika 30 haikuzaa Bao.
Katika Penati hizo, Douglas Costa ndie alieifungia Bayern Penati ya mwisho na ya ushindi.
Guardiola amedumu Bayern kwa Miaka Mitatu ma kutwaa Ubingwa wa Bundesliga kila Mwaka na kuchukua DFB POKAL mara 2.
No comments:
Post a Comment