BUKOBA SPORTS

Wednesday, May 3, 2017

BONANZA LA AFYA KWANZA LAFANA JIJINI ARUSHA

wakwanza kushoto ni muaandaji wa bonanza la Afya kwanza akiwa na timu ya Triple a klabu Fc kabla ya mechi kuanza(habari picha na Woinde Shizza wa libeneke la kaskazini )

Timu ya tigo Fc ikiwa pamoja na timu ya Triple A klabu FC
Timu ya mringa ringa iikiendelea kufanya mazoezi kabla ya kuingia uwanjani
Timu ya wavuta kamba ikiendelea kuvuta kamba

Warembo wakifuatilia mpira kwa makini
Timu ya Triple A wakiwa wanapeana mawazo katika kipindi cha mapunziko
Wadau mbalimbali waliouthuria bonanza hilo wakiendelea kupata vinywaji
Mmoja ya wachezaji wa timu ya Triple A klabu Fc akiwa anatolewa uwanjani na wauguzi mara baada yakuumia wakati akicheza

Timu ya Tigo Fc ikiwa katika picha ya pamoja kabla ya mechi baina yao na timu ya Triple A Klabu Fc kuanza
Na Woinde Shizza,Arusha
Timu ya Triple A klabu imelazimika kutoka sara ya bao moja kwa moja na timu ya Tigo FC katika bonanza la michezo lijulikanalo kwa jina la Afya Kwanza lililofanyika katika viwanja vya Gymkana jijini hapa
Bonanza hilo ambalo ni mara ya kwanza kufanyika limeandaliwa na mkurugenzi wa Bendi ya Rickernest music band ,bendi ambayo makao makuu yake ni jijini hapa na imeshirikisha michezo mbalimbali ikiwemo kuvuta kamba pamoja na mpira wa miguu

Akiongelea bonaza hilo muandaaji wa mashindano hayo Denis Mtedeki alisema kuwa nia rasmi ya kuandaa bonanza hili ni kuwakutanisha watu mbalimbali na kufurahi pamoja pamoja na kushiriki michezo ,ikiwa kama ni sehemu ya kufanya mazoezi
Alisema kuwa bonanza hili limeshirikisha jumla ya timu za mipira wa miguu mbili pamoja na timu zingine mbili ambazo zilifanya kazi ya kuvuta kamba,alizitaja timu hizo kuwa ni timu kutoka kampuni ya simu ya Tigo (Tigo Fc), Olemringaringa FC, Red Apple,Mijada Fc pamoja na Triple a klabu FC.

Denis aliongeza kuwa mbali na kushiriki bonanza hili pia wachezaji na washiriki waliouthuria walipata fursa ya kupima magonjwa mbalimbali ikiwemo kupima presha na kisukari bure.

Aidha aliongeza kuwa bonanza hili alitaishia hapa bali litakuwa likifanyika kila mwisho wa mwezi lengo ikiwa ni kufanya mazoezi ,kuwakutanisha wadau mbambali mbali na kufurahi pamoja

No comments:

Post a Comment