Sanchez akitangazwa kuwa mchezaji mpya wa United, nyota huyo amesema anafuraha kuwa mchezaji wa kwanza kutoka Chile kuichezea klabu kubwa duniani.
Wakati Sanchez akitangazwa na Manchester United, naye mchezaji Henrikh Mkhitaryan ametangazwa na Arsenal kama mchezaji wao mpya, Mkhitaryan amesema kwenda Arsenal ndiyo zilikuwa ndoto zake tangu akiwa mtoto na alitamani siku moja kuitumikia Arsenal kupitia mkataba wa mabadilishano. Wakati huo huo Arsenal imepiga hatua katika kumwania mshambuliaji Pierre-Emerick Aubameyang kutoka Borussia Dortmund.
No comments:
Post a Comment