
Ikicheza huku nyota wao Harry Kane akianzia benchi, alikuwa Fernando Llorente aliyeipatia Tottenham goli la kwanza kwa mpira wa kichwa akiifunga timu yake ya zamani huku akionekana kama ameotea.
Swansea ilishindwa kumudu mashambulizi ya Spurs na katika dakika ya 89, Kane alitoa pande kwa Dele Alli ambaye shuti lake la kwanza liliokolewa na Lukasz Fabianski kabla ya kuukuta mpira na kutumbukiza kimiani.


No comments:
Post a Comment