TIMU ya Kagera Sugar imelazimishwa sare ya 1-1 na Azam FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Kaitaba, Bukoba.
Matokeo hayo yanaiongezea pointi moja Azam FC na kufikisha 34 sawa na mabingwa watetezi, Yanga SC ambao hata hivyo wana mchezo mmoja mkononi.
Kagera Sugar yenyewe inafikisha pointi 14 baada ya kucheza mechi 18 na sasa inajinasua mkiani ikirudi nafasi ya 15 kwa wastani wa mabao tu baada ya kulingana kwa pointi na Njombe Mji FC.
Katika mchezo wa leo, Kagera Sugar walitangulia kwa bao la beki Eladslaus Mfulebe dakika ya 50, kabla ya Iddi Kipagwile kuisawazishia Azam FC dakika ya 53.
Kikosi cha Kagera Sugar kilikuwa: Ramadhani Mohammed, Mwaita Gereza, Eladslaus Mfulebe, Juma Shemvuni, Mohammed Faki, George Kavila/Peter Mwalyanzi dk57, Suleiman Mangoma, Ally Nasoro ‘Ufudu’, Japhary Kibaya/Edward Christopher dk79, Ally Ramadhani na Venance Ludovic/Atupele Green dk69.
Kikosi cha Azam FC: Kipa Razack Abalora, Saleh Abdallah/Iddi Kipagwile dk46, Bruce Kangwa, David Mwantika, Yakub Mohammed, Abdallah Kheri, Stephan Kingue/Paul Peter dk74, Frank Domayo, Salmin Hoza, Mbaraka Yussuph/Ennok Atta Agyei dk46 na Shaaban Idd.
KIKOSI CHA KWANZA
1. Razack Abalora 16
2. Swaleh Abdallah 20
3. Bruce Kangwa 26
4. David Mwantika 12
5. Yakub Mohammed 5
6. Abdallah Kheri 25
7. Stephan Kingue 27
8. Frank Domayo 18
9. Salmin Hozza 22
10. Mbaraka Yusuph 24
11. Shaban Idd 43
Mfumo 3-5-2
WACHEZAJI WA AKIBA
1. Mwadini Ally 1
2. Idd Kipagwile 21
3. Enock Atta 10
4. Benard Athur 9
5. Paul peter 51
6. Oscar Masai 47
7. Masoud Abdallah 15
Kocha Mkuu: ARISTICA CIOABA
Kocha Msaidizi: IDD CHECHE
KAGERA SUGAR
KIKOSI CHA KWANZA
1. Ramadhan Mohammed 30
2. Mwaita Gereza 21
3. Eladslaus Mfulebe 2
4. Juma Shemvuni 25
5. Mohammed Faki
6. George Kavila 15
7. Seleman Mangoma 7
8. Ally Nasoro 6
9. Japhary Kibaya 4
10. Ally Ramadhani 13
11. Venance Ludovic 12
Mfumo 4-4-2
WACHEZAJI WA AKIBA
1. Said Kipao 18
2. Godfrey Taita 20
3. Peter Mwalyanzi 28
4. Paul Ngalyoma 8
5. Pastory Athanas 29
6. Atupele Green 3
7. Edward Christipher 10
Kocha Mkuu: MECKY MEXIME
Kocha Msaidizi: ALLY JANGALU
No comments:
Post a Comment