BUKOBA SPORTS

Tuesday, June 5, 2012

EURO 2012: HAKUNA BINGWA ALIYEWEZA KUTETEA TAJI LAKE MPAKA SASA! JE SPAIN WATAWEZA ??

 
Haijapata kutokea Bingwa wa Mataifa ya Ulaya akafanikiwa kutetea vyema Taji lake na safari hii, huko Nchini Poland na Ukraine kuanzia Juni 8 hadi Julai 1 kwenye Fainali za EURO 2012, Mabingwa wa Ulaya Spain wana nafasi ya kufanya kile walichoshindwa Mabingwa 12 waliowatangulia-KUTETEA VYEMA TAJI LAO LA TAIFA BINGWA BARANI ULAYA!!

Spain wanatinga kwenye EURO 2012 wakiwa pia ni Mabingwa wa Dunia baada ya kutwaa Kombe la Dunia Mwaka 2010 huko Afrika Kusini na wapo Kundi C na Republic of Ireland, Croatia na Italy.
Spain wataanza kutetea Taji lao Juni 10 kwa kucheza na Italia.
Licha ya Bingwa mtetezi kuwa na kibarua kigumu cha kutetea Taji, kitu ambacho hakijawezekana, hata kufika Fainali huwa ni kazi ngumu mno na ni mara moja tu, Miaka 36 iliyopita, Bingwa Mtetezi alimudu kufika Fainali na kutandikwa kwenye Mechi hiyo na kuupoteza Ubingwa wake.

Hao walikuwa ni West Germany ambao walitwaa Ubingwa wa Ulaya Mwaka 1972 na kufungwa Fainali ya Mwaka 1976 na Czechoslovakia.

Bingwa mwingine mtetezi aliekaribia kutetea vyema Taji lake ni Soviet Union ambayo ilikuwa Bingwa Mwaka 1960, Mashindano ya kwanza kabisa ya Mataifa ya Ulaya, lakini kwenye Mashindano yaliyofuata, Mwaka 1964 huko Spain, Soviet Union walifungwa 2-1 na Spain.



HISTORIA YA UBINGWA WA ULAYA:
MWAKA         
MSHINDI          
 HATUA ALIYOFIKA MICHUANO ILIYOFUATA
1960
Soviet Union
MSHINDI WA PILI
1964
Spain
ROBO FAINALI
1968
Italy
ROBO FAINALI
1972
West Germany
MSHINDI WA PILI
1976
Czechoslovakia
MSHINDI WA TATU
1980
West Germany
MAKUNDI
1984
France
HAKUINGIA FAINALI
1988
Netherlands
NUSU FAINALI
1992
Denmark
MAKUNDI
1996
Germany
MAKUNDI
2000
France
ROBO FAINALI
2004
Greece
MAKUNDI
2008
Spain
????????

No comments:

Post a Comment