BUKOBA SPORTS

Monday, April 28, 2014

LIVERPOOL 0 vs CHELSEA 2, MAJOGOO YACHINJWA KWAO ANFIELD!! MOURINHO ACHEKELEA....AJICHUSHA PUMZI NA KUSEMA BADO WANAUSAKA UBINGWA!!

Chelsea wamewapa pigo kubwa Liverpool na ndoto yao ya kutwaa Ubingwa wao wa kwanza katika Miaka 24 na wao kujiwekea matumaini baada ya kushinda Bao 2-0 Uwanjani Anfield wakiwa wamechezesha ‘Kikosi hafifu’ huku jicho lao likiwa kwenye Mechi yao ya Marudiano ya Nusu Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI Jumatano Uwanjani Stamford Bridge.
Mashabiki wa Liverpool walikusanyika kwa ajili ya Mechi hii wakiwa na hakika ya ushindi, hasa baada Jose Mourinho kudokeza atachezesha ‘Kikosi hafifu’, na kabla ya Mechi kuanza Basi lililobeba Wachezaji wa Liverpool lilipokuwa kwa shangwe kubwa nje ya Anfield mithili ya Paredi ya Ubingwa.

Bao zilizoiua Liverpool zilifungwa na Demba Ba katika Dakika ya 45 baada ya Nahodha Steven Gerrard kuteleza na Demba Ba kunufaika na kwenda kufunga na la Pili kupigwa Dakika za Majeruhi na Willian, alietokea Benchi, alipopokea Pasi murua ya Fernando Torres.

Ushindi huu umewaacha Chelsea wakiwa Pointi 2 nyuma ya Vinara Liverpool lakini huenda matokeo haya yakawanufaisha sana Manchester City ambao wana Mechi mbili mkononi na wakishinda zote wataikamata Liverpool na kuongoza kwa Ubora wao wa Magoli.Mashabiki wa Liverpool wakionesha sapoti yao kwa kocha waoKipute kimeanza...Kama kawaida yake Jose!! kocha wa Makeke!!Wachezaji wa Liverpool wakimzunguka kocha Jose Mourinho.Steven Gerrard akitaka mpira kutoka kwa Jose!Patashika uwanjani!!Ashley Cole wa Chelsea na Raheem Sterling wakiutafuta mpira kwa nguvu..Leo siku mbaya kwetu!! Kocha wa Liverpool Brendan RodgersBa ndie alieziona nyavu wa kwanza.Asante! Ba akiomba baada ya kufunga bao!
Mapenzi bado yapo!!! Kocha wa zamani wa Liverpool Kenny Dalglish akionesha kuchukia baada ya timu ya Liverpool kupoteza!!William ndie alieongeza bao la pili na kufanya 2-0 dhidi ya wenyeji Liverpool2-0Liverpool hoi....taabaniSiku mbaya!!!

No comments:

Post a Comment