BUKOBA SPORTS

Sunday, April 27, 2014

EPL, SUNDERLAND 4 v CARDIFF CITY 0, SUNDERLAND YAJIKWAMUA MKIANI, YAPANDA JUU BAADA YA KUTEMBEZA KICHAPO!

WAKICHEZA kwao Stadium of Light jana, Sunderland wameitwanga Cardiff City Bao 4-0 na wao kujinasua toka mkiani mwa Ligi Kuu England na kuwatupa Cardiff huko mkiani.
Sunderland walipata Bao la Kwanza katika Dakika ya 26 Mfungaji akiwa Connor Wickham na Fabio Borini kufunga kwa Penati ya Dakika 45 iliyosababishwa na Rafu kwa Connor Wickham toka kwa Juan Cala ambae alitolewa nje kwa Kadi Nyekundu.
Breakthrough: Connor Wickham celebrates the header that put Sunderland up 1-0
Emanuele Giaccherini aliifungia Sunderland Bao la Tatu katika Dakika ya 76 na Connor Wickham kupachika Bao la 4 katika Dakika ya 86.



Wickham CHUPUCHU afunge bao...mpira uligonga posti

Patashika langoni!!

Wickham akishangilia bao lake

Wickham akipongezwa na Sebastian Larsson

No comments:

Post a Comment