BUKOBA SPORTS

Wednesday, January 28, 2015

AFCON 2015: ALGERIA, GHANA ZATINGA ROBO FAINALI, ANDRE AYEW AIPA USHINDI GHANA! SOUTH AFRICA NA SENEGAL SAFARI IMEISHIA HAPO!

KUNDI C la Mashindano ya Mataifa ya Afrika, AFCON 2015, limemaliza Mechi zao za mwisho na Algeria na Ghana kutinga Robo Fainali huku Senegal na South Africa wakibwagwa nje.
Ghana walitoka nyuma kwa Bao 1-0 na kuichapa South Africa Bao 2-1 katika Mechi ya Kundi C la AFCON 2015.
South Africa walipata Bao katika Dakika ya 17 baada ya Mandla Masango kufuatia uzembe wa Ghana kuosha Mpira uliotumbukizwa ndani ya Boksi.
Hadi Mapumziko South Africa 1 Ghana 0.
Kipindi cha Pili Ghana walicharuka na hatimae kupata Bao Dakika ya 73 Mfungaji akiwa John Boye na kuongeza la pili kupitia Andre Ayew kwa Kichwa Dakika ya 83 alipounganisha Mpira wa Baba.
Ghana wamesonga Robo Fainali wakiwa Washindi wa Kundi C na watacheza na Mshindi wa Pili wa Kundi D.

No comments:

Post a Comment