BUKOBA SPORTS

Tuesday, January 20, 2015

FA CUP RAUNDI YA NNE, MAN UNITED UWANJANI IJUMAA, KIPA MPYA VICTOR VALDES KULINDA LANGO KWA MARA YA KWANZA DHIDI YA CAMBRIDGE UNITED.

Kipa wa Manchester United, Victor Valdes, ambae ni Nguli wa Barcelona na Timu ya Taifa ya Spain, anatarajiwa kuichezea kwa mara ya kwanza kabisa Klabu yake mpya hapo Ijumaa Usiku kwenye Mechi ya Ugenini ya Raundi ya 4 ya FA CUP dhidi ya Cambridge United.
Valdes, mwenye Miaka 32 ambae ni Mchezaji wa Kimataifa wa Spain, amesaini kuichezea Manchester United kwa Mkataba wa Miezi 18 Wiki iliyopita na amekuwa akifanya Mazoezi na Timu hiyo kwa Miezi miwili sasa katika harakati zake za kurudia hali yake ya kawaida baada ya kuumia vibaya Goti lake Mwezi Machi.
Akiwa na Barcelona, Valdes alitwaa Ubingwa wa La Liga mara 6 na UEFA CHAMPIONS LIGI mara 3 na kabla Msimu uliopita kumalizika alitangaza kuondoka Barca baada ya mwenyewe kukataa kuongeza Mkataba wake.
Cambridge United, ambayo inacheza Ligi 2, ndio Timu pekee ya Daraja la chini kabisa iliyobakia kwenye Raundi ya 4 ya FA CUP na Mechi hii itakayochezwa Uwanjani kwao Abbey Stadium huko Cambridge ni ya Kihistoria kwao ingawa waliwahi kufika Robo Fainali ya FA CUP mara mbili katika Miaka ya 1990 na 1991.
wenye Msimamo wa Ligi 2, Cambridge United wako Nafasi ya 12.

No comments:

Post a Comment