Kwenye Mechi hiyo ambayo Chelsea waliifunga Liverpool 1-0 na kutinga Fainali, Costa ameshitakiwa kwa kumtimba kwa makusudi Beki wa Liverpool Emre Can katika Dakika ya 12 ya Mechi hiyo.
Ikiwa atakiri Kosa lake, Costa atafungiwa Mechi 3 kuanzia ya Jumamosi dhidi ya Mabingwa wa England, Manchester City, Uwanjani Stamford Bridge.
Costa amepewa hadi Alhamisi Januari 29, Saa 3 Usiku kukana au kukiri Kosa.
No comments:
Post a Comment