Sunday, March 13, 2016

FULL TIME: ASTON VILLA 0 v 2 TOTTENHAM HOTSPURS, HARRY KANE ATEMA CHECHE!

BAO mbili za Harry Kane dakika ya 45 na 48' zimewapa ushindi wa bao 2-0 leo kwenye Uwanja wa Villa Park dhidi ya Wenyeji wao Aston Villa.2-0Ushindi huo umeifanya Spurs iwe Pointi 2 nyuma ya Vinara Leicester City lakini wao wamecheza Mechi 1 zaidi.
Kesho Usiku Leicester wako kwao King Power Stadium kucheza na Newcastle ambayo ni ya pili toka mkiani lakini sasa wana Meneja mpya, Rafa Benitez, anaeanza kazi yake mpya rasmi hiyo kesho baada ya kupewa wadhifa huo Juzi alipotimuliwa Steve McClaren.VIKOSI:
Aston Villa:
Guzan, Hutton, Okore, Lescott, Cissokho, Veretout, Gana, Westwood, Gil, Ayew, Gestede
Akiba: Bunn, Richards, Clark, Bacuna, Sinclair, Green, Lyden
Tottenham: Lloris, Walker, Alderweireld, Wimmer, Rose, Dier, Dembele, Lamela, Eriksen, Alli, Kane
Akiba: Vorm, Trippier, Davies, Carroll, Mason, Chadli, Son

No comments:

Post a Comment