BUKOBA SPORTS

Sunday, December 31, 2017

EPL FULL TIME...WEST BROM 1-1 ARSENAL

FULL TIME: CRYSTAL PALACE 0-0 MANCHESTER CITY

Baada ya kushinda michezo 18 mfululizo ya Ligi Kuu ya Uingereza, hatimaye Crystal Palace imefanikiwa kusimamisha rekodi ya ushindi wa Manchester City hii leo.
Crystal Palace licha ya kutoa sare tasa na vinara wa ligi Manchester City, pia ingeweza kuibuka na ushindi wa goli moja lakini kipa Enderson aliwanyima ushindi. 


Palace walidhani kuwa wataibuka na ushindi baada ya kupata penati dakika za mwisho baada ya kuangushwa Wilfred Zaha lakini penati ya Luka Milivojevic ilipanguliwa.
Licha ya kutibuliwa rekodi ya ushindi mfululizo Manchester City pia imejikuta ikikumbwa na hofu ya majeruhi baada ya Kevin De Bruyne na Gabriel Jesus kuumia.
Raheem Sterling akimuangusha katika eneo hatari Wilfred Zaha na muamuzi kuamua mkwaju wa penati
Luka Milivojevic akishuhudia mpira wa penati aliyoipiga ukizuiliwa kwa miguu na kipa Enderson wa Manchester City

MANCHESTER UNITED WATOKA SARE TENA MBELE YA SOUTHAMPTON 0-0

Paul Pogba akiwa chini akilalamika juu ya goli alilolifunga na kuambiwa na mwamuzi kuwa alikuwa kaotea dhidi ya Southampton na kutoka 0-0.
Pogba Akimwangaisha kipa wa Southampton jana usiku

Marcus Rashford akiendesha mpira mbele ya mchezaji wa Southampton.
Shane Long  akiwana mlinda lango David de Gea  ana kipa huyo kuokoa mpira ambao ulikuwa uzame langoni.

chupuchupu!
Long akipagawa kwa kutofunga bao
Jose Mourinho akiwaangalia Vijana Old Trafford
Kipa Alex McCarthy akiokoa mpira langoni mwake
McCarthy alibadilishwa na nafasi yake kutoka kwa Fraser Forster Pogba stands akimwangalia Pierre-Emile Hojbjerg baada ya kuanguka chini.
Romelu Lukaku alipata tatizo na kuumia baada ya kukutana uso kwa uso na  Wesley Hoedt wakigombea mpira wa kichwa.

Lukaku kiwa chini akiugulia jeraha.

Lukaku akiwa hoi!
Juan Mata

Luke Shaw akimwekea kifua Dusan Tadic

LIVERPOOL 2 vs 1 LEICESTER CITY, MOHAMED SALAH AIBEBA LIVERPOOL NYUMBANI!


Raia wa Misri Mohamed Salah amefunga magoli mawili na kuisaidia Liverpool kuongeza rekodi yao ya kutofungwa katika michezo 15 kwenye michuano yote baada ya kuibuka na ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya Leicester City.
Katika mchezo huo uliopigwa kwenye dimba la Anfield Jamie Vardy aliwapatia wageni goli la kuongoza akiitumbukiza kiulani pasi ya Riyad Mahrez goli lililoduma hadi kipindi cha pili pale Salah alipoisawazishia Liverpool.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Misri baadaye tena alimzungusha Harry Maguire na kuachia shuti lililojaa wavuni na kuandika goli la pili na kufikisha magoli 17 katika michezo ya Ligi Kuu ya Uingereza katika msimu huu.


Mshambuliaji nyota wa Leicester City akifunga goli la kwanza katika mchezo huo

Mshambuliaji nyota wa Liverpool Mohamed Salah akifunga goli la kusawazisha kabla ya baadaye kuongeza la pili

CHELSEA YAFUNGA MWAKA 2017 KWA KWA KUINYUKA STOKE CITY BAO 5-0, WAPANDA NAFASI YA PILI

Timu ya Chelsea imeendeleza wimbi la ushindi katika Ligi Kuu ya Uingereza baada ya hii leo kuibuka na ushindi wa kishindo wa magoli 5-0 dhidi ya Stoke City na kumaliza mwaka 2017 kwa ushindi.
Katika mchezo huo wenyeji Chelsea walifunga goli la kwanza kupitia kwa Antonio Rudige kufuatia krosi ya Mbrazil Willian kisha baadaye Danny Drinkiwater akaongeza goli la pili kisha Pedro akafunga la tatu.
Willian aliongeza goli la nne kwa mkwaju wa penati baada ya kuchezewa rafu na Geoff Cameron na katika dakika ya 88 Zappacosta akakamilisha karamu ya magoli kwa kufunga goli lake la kwanza katika Ligi Kuu ya Uingereza.
Antonio Rudige akifunga goli la kwanza la Chelsea katika mchezo huo

Danny Drinkwater akifunga kwa shuti la kuubetua mpira kwenye kona ya goli.

Friday, December 29, 2017

KOCHA ARSENE WENGER HANA WASIWASI YA KUMKOSA SANCHEZ ANAYEONDOKA JANUARI, WASHINDA BAO 3-2 DHIDI CRYSTAL PALACE.


Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger, amesema kuwa hana wasiwasi wa kumpoteza Alexis Sanchez Januari licha ya mshambuliaji huyo kufunga mara mbili wakati timu yake ikiibuka na ushindi wa magoli 3-2 dhidi ya Crystal Palace.
Crystal Palace ilisawazisha goli kupitia kwa Andros Townsend baada ya Shkodran Mustafi kufunga goli la kwanza katika mchezo huo na kisha baadaye katika kipindi cha pili akafunga mawili kwa muda wa dakika nne.
Crystal Palece ilipata goli la pili katika kupitia kwa James Tomkins kwa mpira wa kichwa, hata hivyo walishidwa kusawazisha la tatu na kuifanya Arsenal iliyokatika nafasi ya sita kuwa na pinti sawa na Tottenham iliyonafasi ya tano.
Mchezaji wa Arsenal Shkodran Mustafi akifunga goli la kwanza katika mchezo huo
Mshambuliaji Andros Townsend akifunga goli la kusawazisha na kufanya matokeo kuwa 1-1
Alexis Sanchez akifunga goli lake la pili katika mchezo huo na kufanya matokeo kuwa 3-2

WASANII ASLAY NA NANDY WATUA BUKOBA LEO HII, TAYARI KWA SHOW YA MIAKA 9 YA KASIBANTE REDIO KWENYE UKUMBI WA ST. THEREZA KESHO 30/12/2017

Wasanii wa Muziki wa Bongo Flava, Aslay (Katikati) (kulia ni Nandy na kushoto ni Chiba muda mfupi baada ya kutua kwenye Uwanja wa Ndege Mjini Bukoba.
Kesho Jumamosi wanatarajiakuangusha bonge la show kwa wakazi wa Manispaa ya Bukoba pale ukumbi wa St.Theresa karibu na banki ya NMB.
Show hiyo ni moja ya maadhimisho ya miaka 9 ya uwepo wa Kasibante Fm Radio Bukoba tangu kuanzishwa kwake.
Show hiyo itaanza majira ya saa moja jioni hadi majogoo huku Wheel Steel ikisimamiwa na DJ`s kutoka Pro24Tanzania.
Mmiliki wa www.bukobasports.com Faustine Ruta (kulia) akiwa na Aslay (kushoto).


Msanii Nandy (kushoto) akiwa na Faustine Ruta

Baadhi ya Waandishi wa Habari wa Redio Kasibante FM 88.5 wakiwa picha ya pamoja.

Wednesday, December 27, 2017

CONTE ASEMA KUKOSA BAHATI KUMEWAFANYA WASHINDWE KUWAFIKIA MAN CITY, MAN UNITED SARE TENA!

Kocha Antonio Conte amesema ni kukosa bahati tu kulioifanya timu yake wa Chelsea kuwa pointi 13 nyuma ya vinara wa ligi Manchester City baada ya kuifunga Brighton 2-0.
Chelsea imepata ushindi wa sita mfululizo katika Ligi Kuu ya Uingereza baada ya jana kusakata kandanda safi na kupata magoli hayo kupitia kwa Alvaro Morata na Marcos Alonso.

Alvaro Morata akifunga kwa mpira wa kichwa goli la kwanza la Chelsea
Shuti la Jesse Lingard limeinyima Burnley kupata ushindi katika dimba la Old Trafford na kutoka sare ya magoli 2-2 matokeo ambayo yanafifisha matumaini ya kukimbiza ubingwa.

Katika mchezo huo Ashley Barnes aliwafungia wageni goli la kwanza na kisha baadaye Steven Defour akafunga goli la pili na kufanya hadi mapumziko matokeo kuwa 2-0.
Jesse Lingard akiachia shuti na kuisaidia Manchester United kulazimisha sare dhidi ya Burnley

FIRMINO AFUNGA MAWILI WAKATI LIVERPOOL IKICHAPA BAO 5-0 SWANSEA FC


Roberto Firmino amefunga magoli mawili wakati Liverpool ikiichapa Swansea isiyonakocha na iliyomkiani kwa magoli 5 bila majibu katika mchezo wa Ligi Kuu ya Uingereza Katika mchezo huo Philippe Coutinho alifunga goli la kwanza baada ya kunasa pasi ya Mohamed Salah, kabla ya Firmino kufunga la pili na Trent Alexander-Arnold la tatu.
Roberto Firmino aligongeza goli la tatu kisha baadaye Oxlade-Chamberlain akamalizia karamu ya magoli kwa kufunga goli la tano.


Roberto Firmino akimalizia kiulaini pasi iliyozaa goli ya Mohamed Salah

Oxlade-Chamberlain akiachia shuti na kufunga goli la tano katika mchezo huo

Monday, December 25, 2017

MERRY CHRISTMAS TO YOU


On behalf of everyone who makes www.bukobasports.com what it is, I want to wish you A Merry Christmas.

ROBERTO FIRMINO AIOKOA LIVERPOOL DAKIKA ZA MWISHO NA KUTOKA SARE NA ARSENALYA GOLI 3-3


Goli la shuti kali la Roberto Firmino limeisaidia Liverpool kutoa sare katika mchezo mzuri wa Ligi Kuu ya Uingereza ulioshuhudia Arsenal ikifunga magoli matatu ndani ya dakika tano za kipindi cha pili.
Arsenal ilikuwa nyuma kwa magoli 2-0 yaliyofungwa na Philippe Coutinho aliyefunga goli la kwanza kwa mpira wa kichwa kabla ya raia wa Misri Mohamed Salah kuongeza goli la pili katika kipindi cha pili.
Lakini hafla Arsenal walizinduka na kufunga goli la kwanza kupitia kwa Alexis Sanchez akifunga kwa mpira wa kichwa krosi ya Hector Bellerin, kabla ya Granit Xhaka kutumbukiza la pili kisha Mesuit Ozil kufunga la tatu.


Philippe Coutinho akifunga goli kwa mpira wa kichwa hii ikiwa ni mara ya kwanza kwa mchezaji huyo kufunga goli kwa mpira wa kichwa katika Ligi Kuu ya Uingereza

Mohamed Salah akifunga goli la pili la Liverpool kwa shuti lililomshinda kipa wa Arsenal

Alexis Sanchez akiifungia Arsenal goli la kwanza lililoamsha ari ya kusawazisha magoli waliyofungwa na kuongeza moja

Roberto Firmino akiisawazishia Liverpool goli la tatu na kufanya mchezo huo kumalizika kwa sare ya magoli 3-3